MFUKO WA UINJILISHAJI

NYUMBANI KUHUSU SISI MISHENI YETU NIA ZA SALA MAWASILIANO CHANGIA SASA
Hero Background
JIMBO KUU KATOLIKI ARUSHA

TUIPELEKE INJILI
KATIKA JAMII

Mchango wako ni mbegu ya neno la Mungu. Tusaidie kufikia jamii za Wamasai, kulea vijana, na kueneza upendo wa Kristo kila kona ya Arusha.

Worship in Arusha
Neno la Askofu

Kuhusu Mfuko wa Uinjilishaji

Uinjilishaji ni kwa kila Mbatizwa; Kuinjilisha ni kufikisha Neno kwa maeneo husika yenye uhitaji pasipo kujali kabila wala rangi. Hivyo wote tunawajibika kuifanya kazi ya Uinjilishaji.

Mhashamu Askofu Mkuu Isaac Amani Jimbo Kuu Katoliki Arusha

Majukumu ya Mfuko wa Uinjilishaji

Ujenzi na Miundombinu

Kujenga na kuendeleza misioni mpya, vigango, parokia, pamoja na ununuzi wa ardhi kwa ajili ya upanuzi wa Kanisa katika maeneo yenye uhitaji.

Kuwezesha Wahudumu wa Injili

Kusaidia gharama za usafiri na kutoa mafunzo kwa Mapadri, Watawa, na Makatekista ili waweze kulifikisha Neno la Mungu vijijini na pembezoni.

Vifaa vya Kuinjilisha na Vitendea Kazi

Kusambaza Biblia Takatifu, Misale, Katekisimu, na visakramenti; ikiwemo pia kununua vyombo vya usafiri (Magari, Pikipiki) kurahisisha huduma za kichungaji.

Mawasiliano na Utangazaji wa Neno

Kuandaa vipindi vya kidini kwenye Redio, TV, na mitandao ya kijamii, pamoja na kugharamia semina na makongamano ya kiinjilishaji kwa umati mkubwa.

Kutegemeza Misioni

Kusaidia uendeshaji wa vigango, na parokia changa pamoja na kuwekeza katika miradi inayoleta tija katika kuliimarisha Kanisa kijamii na kiuchumi.

0M+
Michango (2025)
0
Miradi Iliyofadhiliwa
0M+
Thamani ya Ufadhili
0%
Asilimia ya Ubia
Matunda ya Michango Yako

Miradi Iliyofadhiliwa 2025

Kupitia michango yenu, Mfuko umefanikiwa kufadhili miradi 14 kwa asilimia 60% yenye thamani ya TZS Milioni 224.3. Hapa kuna baadhi ya miradi hiyo mikubwa:

Usafiri kwa Wamishenari

Tumewezesha ununuzi wa pikipiki na matengenezo ya magari kwa parokia za pembezoni ikiwemo Matui, Ngorongoro, na Mto wa Mbu ili kurahisisha uinjilishaji.

Makanisa na Makazi

Ujenzi wa Kanisa Kigango cha Samunge (Mt. Yuda Tadei), Parokia ya Hippo, na ujenzi wa nyumba za mapadri Mbuguni na Simanjiro Kaskazini.

Sauti ya Injili Hewani

Kusaidia uendeshaji wa vipindi na miundombinu ya AMANI Radio FM kwa ufadhili wa TZS Milioni 59.4 ili injili iwafikie wengi zaidi popote walipo.

Ushuhuda Kwa Picha

Tazama pikipiki mpya kwa ajili ya wamishenari vijijini

Pikipiki Madhabahuni

Ununuzi wa Pikipiki

Kusaidia uinjilishaji vijijini.

Pikipiki Karibu

Usafiri Imara

Kufikia kila muumini.

Pikipiki Viroba

Pikipiki Mpya

Matunda ya michango yenu.

Uchimbaji Wa Visima Vya Maji

Huduma ya maji safi na salama kwa jamii zetu

Visima vya Maji

Ujenzi Wa Makanisa Na Makazi

Hatua za ujenzi zinazoendelea kutokana na michango ya waumini

Kanisa 1

Kigango cha Samunge

Ndani ya Kanisa

Kanisa 2
Kanisa 3
Kanisa 4
Nyumba ya Mapadri

Nyumba ya Mapadri

Imekamilika Asilimia 100

Kigango cha Samunge

Kigango cha Samunge

Ujenzi Unaendelea

Makazi Ujenzi Green
Makazi Ujenzi Red
Makazi Kamilika Red

Makazi ya Mbuguni

Mradi uliokamilika kikamilifu

Utume Wa Pembezoni

Mapadri wakitoa huduma za kiroho katika jamii za wafugaji na vijijini

Misheni kwa Wamasai

Misheni kwa Wamasai

Engaruka, Arusha

Utume Vijijini
Misa Chini ya Miti
Kuhubiri Neno
Lengo Letu la 2026

Tuvuke Pamoja Kufikia Lengo la TZS 842.6 Milioni

Kila mchango wako unaofanya kupitia mtandao wa simu unatuwezesha kufikia asilimia kubwa ya lengo hili. Chagua kiwango chako leo na uwe Balozi wa Uinjilishaji!

Injili Kijijini

TZS 5,000

Inasaidia kutoa kijitabu kimoja cha mafunzo ya dini kwa kijana mmoja mkoani.

Changia Hapa
Inapendekezwa

Misheni ya Upendo

TZS 50,000

Inasaidia safari ya misheni ya siku moja kwa makatekista vijijini kwa ajili ya ubatizo.

Changia Hapa

Uinjilishaji Dijitali

TZS 100,000

Inachangia uendeshaji wa promosheni ya kimtandano kwaajili ya mfuko, kama youtube adds, sms bulk push.

Changia Hapa

Kikokotoo cha Matokeo ya Mchango wako

Buruta kielekezi chini kuona jinsi mchango wako unavyosaidia misheni yetu kijamii.

TZS 5,000 TZS 100,000 TZS 250,000 TZS 500,000
KIASI CHA MCHANGO TZS 50,000
MATOKEO YA MCHANGO WAKO

Inagharimia mafuta ya gari la safari ya misheni ya dharura vijijini.

1 Jinsi ya Kuchangia

m-pesa
Vodacom M-Pesa
  1. 1. Piga *150*00#
  2. 2. Chagua 4 Lipa bill
  3. 3. Chagua 4 Ingiza namba ya kampuni
  4. 4. Namba ya kampuni: 770700
  5. 5. Kumbukumbu: Namba ya Parokia
  6. 6. Weka kiasi 1000 au zaidi
  7. 7. Ingiza namba ya siri
  8. 8. Chagua 1 kuthibitisha
a
airtel money
Airtel Money
  1. 1. Piga *150*60#
  2. 2. Chagua 5 Lipa bill
  3. 3. Chagua 4 Ingiza namba ya kampuni
  4. 4. Namba ya kampuni: 770700
  5. 5. Weka kiasi 1000 au zaidi
  6. 6. Kumbukumbu: Namba ya Parokia
  7. 7. Ingiza namba ya siri
  8. 8. Chagua 1 kuthibitisha
yas
Mixx by Yas
  1. 1. Piga *150*01#
  2. 2. Chagua 4 Lipa bill
  3. 3. Chagua 3 Ingiza namba ya kampuni
  4. 4. Namba ya kampuni: 770700
  5. 5. Kumbukumbu: Namba ya Parokia
  6. 6. Weka kiasi 1000 au zaidi
  7. 7. Ingiza namba ya siri
  8. 8. Chagua 1 kuthibitisha
halo pesa
HaloPesa
  1. 1. Piga *150*88#
  2. 2. Chagua 4 Lipa bill
  3. 3. Chagua 3 Ingiza namba ya kampuni
  4. 4. Namba ya kampuni: 770700
  5. 5. Kumbukumbu: Namba ya Parokia
  6. 6. Weka kiasi 1000 au zaidi
  7. 7. Ingiza namba ya siri
  8. 8. Chagua 1 kuthibitisha
Akaunti ya Benki

MKOMBOZI BANK

01211520778901

Jina: CATHOLIC ARCHDIOCESE OF ARUSHA - UINJILISHAJI

TUMIA NAMBA: 58 KWA WALE WASIO MAPAROKIANI NA WENYE MAPENZI MEMA.

Scan Kulipia

Scan hapa kwa kufuata njia za uchangiaji.

"Mungu ampenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu."

2 Wakorintho 9:7

Thibitisha Mchango Wako

Ukishatuma mchango wako kwa M-Pesa, Airtel, Tigo au Benki, jaza taarifa hapa chini ili tukutambue na kukuandikia risiti rasmi ya shukrani.

Sauti za Imani

Ushuhuda kutoka kwa wale wanaoguswa na kazi yako ya uinjilishaji.

"Mfuko huu umesaidia sana kufikisha neno la Mungu katika maeneo ambayo awali yalikuwa magumu kufikika. Tunaona mabadiliko makubwa ya kiroho kwa watu wetu."

Padre Francis

Padre Francis

Misheni ya Engaruka

"Kama kijana, nimepata nafasi ya kukua kiroho kupitia mafunzo na semina zilizofadhiliwa na Mfuko wa Uinjilishaji. Tunamshukuru Mungu kwa kila anayechangia."

Maria Lowassa

Maria Lowassa

Umoja wa Vijana

"Mafunzo niliyopata yamenisaidia kuwa katekista bora. Sasa naweza kuwafundisha watoto na watu wazima neno la Mungu kwa ufasaha zaidi."

Yohane Mollel

Yohane Mollel

Makatekista Arusha

Shuhudia Kazi ya Misheni

Mawasiliano na Altare

Tuma Nia Yako
ya Sala

Kila mchango wako unaambatana na baraka. Mbali na kusaidia ujenzi na maendeleo ya kiroho, tunapenda kuungana nawe katika sala. Tuma nia yako maalum ya sala hapa chini, na mapadri wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha wataziweka nia hizi katika Ibada ya Misa Takatifu.

Sadaka ya Ibada

Nia zako zinasomwa na kuwekewa ibada maalum katika makao makuu yetu ya Jimbo.

Usiri Kamili wa Nia yako

Unaweza kuchagua kutaja jina lako au kutuma nia yako kama siri (Anon). Mungu anaijua mioyo yote.

"Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa."

— Mathayo 7:7

Ombi la Sala / Nia Maalum

"Mimi hapa, Nitume Mimi."

— Isaya 6:8

Wasiliana
Nasi Leo

Una swali au unataka kujua zaidi kuhusu kazi yetu? Tuandikie ujumbe hapa.

Ofisi Yetu

Arusha, Tanzania

Tupigie

+255 652 391 121